Friday, May 11, 2012

Imewezekana Mtwara na Lindi, kwingine je?

HPIM7143

Hapo ni Nanyumbu, Mtwara

Hivi Mtwara na Lindi si Tanzania ama?

Katika sehemu mbalimbali nchini unakotumika usafiri wa pikipiki almaarufu bodaboda usalama wa abiria si ishu sana kwani ni dereva tu anayetakiwa kuvaa kofia.

Katika mkoa wa Lindi na Mtwara kofia kwa mteja ni lazima…tembea wilaya zote za mikoa hiyo utajionea. Ukipanda tu anakushikisha anakwambia ‘vaa kofia kwa kuwa tukikamatwa utatozwa sh 40,000 kama faini’. Kama hana kofia ya abiria mkikutwa analipa na wewe unalipa kwa kukubali kupanda bodaboda isokuwa na kofia.

Changamoto huko ni kuwa KOFIA hizo zinazovaliwa na kila mtu, kiafya inakaaje hiyo?

Wednesday, May 9, 2012

Walinda nchi ndo Wavunja nchi, si ndiyo?

mshikaki-wavunja nchi

Picha hii inaonesha jinsi wanaopaswa kuhakikisha kuwa haki, amani na sheria zinalindwa na kutekelezwa wao ndo wa kwanza kuzivunja. Mshikaki wa nguvu huo!!!

Monday, May 7, 2012

Wanakijiji wanajikamua weeeeee, kisha mambo yanageuka!

SAM_0509

japo sitaliweka hapa kipicha….ni jengo zuri hapa kijiji cha Mchinga 1………lilojengwa kwa ajili ya kutumika kama kituo cha polisi likiwa na vyumba vya kuhifadhia wahalifu.

lakini tangu jengo limalizike hadi leo hakuna cha polisi ama mgambo hapo kituoni….

matokeo yake kukitokea mhalifu kijijini, kwa amri ya mtendaji wa kijiji mtu huswekwa humo na kwa uamzi wake hupelekwa mahakamani-mahakama iliyoko pembeni ya jengo hilo. Picha ya jengo la mahakama ni hiyo hapo chini.

Friday, May 4, 2012

Bendera ya Taifa haiheshimiki tena?

Nijuavyo bendera ya taifa hupandishwa saa 12 asubuhi na kushushwa saa 12 kamili jioni.

Hapa ni mahakama ya mwanzo ya Mchinga 1 katika wilaya ya Lindi.

SAM_0507

Tangu saa 12 kamili jioni nilikuwa hapa kutizama kama naweza kubana miguu kwa heshima ya kushushwa kwa bendera ya taifa iliyoko mbele ya mahakama hii.

SAM_0508

Mpaka saa 12 na robo ilikuwa bado haijashushwa….

na ilipofika saa 12.16 mtu akajongea kuishusha…na akanionesha ishara ya ushushwaji wa bendera (sio filimbi kupulizwa)!

SAM_0510

Wazo likanijia…labda huku kigezo si muda bali GIZA ndo linaamua kama ipandishwe ama ishushwe.

Uswazi kuna mambo!!!!

Friday, April 20, 2012

Ni za Ukweli japo sina uhakika nazo!

HPIM7145

Ina uwezo wa kwenda kijijini na upasuaji ukafanyika humo! Moja iko Hospitali ya Mkoa wa Mara..sijui kwa nini haiendi vijijini.

Nyingine nimeikuta Hospitali ya wilaya ya Tandahimba, na hii hapa ni ya wilaya ya Nanyumbu mkoa wa Mtwara.

Wednesday, April 18, 2012

Ni kweli?

HPIM7152

Kiuhalisia haiko hivi!

Monday, April 16, 2012

Baadhi ya Wilaya Mpya zinafaidi sana!

HPIM7181

Hii ni nyumba ya DC wa Nanyumbu

HPIM7180

Hii ni ofisi ya DC wa Nanyumbu

HPIM7154

Hapa ni Halmashauri ya wilaya ya Nanyumbu

Mbali na majengo hayo ya ngugu kihivyo watumishi wa halmashauri wamejengewa nyumba za kuishi ambazo kiukweli ni nzuri sana…

Majengo kama haya ya maDC nimeyakuta katika Halmashauri ya Liwale, Ruangwa (H/shauri) Newala na  Tandahimba

Natumai hatatokea Mkapa mwingine aziuze kwa bei ya bwerere!